Saturday, March 19, 2016

KUELEKEA WIKI YA KINYWA NA MENO MACHI 20 , MADAKTARI WATEMBELEA NYUMBA YA WATOTO YATIMA MGOLOLE

Makamu wa Rais wa chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno na Dk, Bingwa wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Dk. Ambege Mwakatobe akimuangalia Kinywa mtoto Ferdinandi Chales (1) wakati wa kuelekea Madhimisho ya Afya ya Kinywa na Meno yatakayo fanyika kesho machi 20, 2016. 
Daktari Bingwa wa Afya ya Kinywa na Meno Hospitali ya Taifa Muhimbili Dk. Deogratias Kilasara akimfanyia ukaguzi wa Kinywa na Meno, Godfey Mikael (10) wakati walipotembelea kituo cha Nyumba ya watoto Yatima Mgolole Mkoani Morogoro katika kuelekea Maadhimishoa ya Kilele cha Maadhimisho hayo machi 20, ambapo Kitaifa yatafanyika Mkoani humo
Mmoja wa Walezi wa Watoto wa liyopo kituo cha Nyumba ya watoto Yatima Mgolole Mkoani Morogoro, Filbertha Kunambi (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na watoto hao, ambapo na yeye alilelewa kituoni hapo na hadi sasa ametimiza miaka 50 bado ana pata huduma mbalimbali kituoni hapo
  Makamu wa Rais wa chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno na Dk, Bingwa wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Dk. Ambege Mwakatobe aliyevaa kofia akiwa katika picha ya pamoja na madaktari wenzake, walezi na watoto mara walipotembelea kituoni hapo katika wiki ya kinywa na meno Duniani ambapo Kitaifa yatafanyika Mkoani Morogoro machi 20, 2016


Makamu wa Rais wa chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno na Dk, Bingwa wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Dk. Ambege Mwakatobe akiwa eneo la tukio kwenye uwanja wa Shule ya Msingi K. Ndege Sabasaba Morogoro, ambapo Shughuli za Maadhimisho ya Kilele cha Afya ya Kinywa na Meno yatakapo fanyikia Machi 20, 2016.
(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)


No comments:

Post a Comment