Wednesday, March 23, 2016

DAWASA YATOA DARASA KWA VIONGOZI WA JUMUIYA 15 ZA WATUMIA MAJI DAR ES SALAAM, KIBAHA NA BAGAMOYO.

Meneja Uhusiano wa Jamii wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASA) Bi.Neli Msuya akizungumza na viongozi wa Jumuiya 15 za Watumia Maji zilizojengwa chini ya mradi wa Maji Yetu uliofadhiliwa na Serikali ya Ubelgiji uliogharimu shilingi Bilioni 14.5 alipokutana nao leo jijini Dar es salaam.
Mshauri wa Ufundi wa DAWASA –BTC Mhandisi Praygod Mawalla akitoa elimu kwa viongozi wa Jumuiya 15 za Watumia Maji katika jiji la Dar es salaam namna ya kuifanya miradi wanayoisimamia ijiendeshe na kuwa endelevu kwa manufaa ya wananchi.

Mshauri wa Ufundi wa DAWASA –BTC Manjolo Kambili akitoa akitoa ufafanuzi kuhusu Programu ya za utoaji wa mafunzo kwa watumiaji wa Maji katika maeneo yenye miradi hiyo wakati wa mkutano na viongozi wa Jumuiya 15 za Watumia Maji za jiji la Dar es salaam.

Viongozi wa Jumuiya 15 za Watumia Maji zilizojengwa chini ya mradi wa Maji Yetu wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa na watendaji wa DAWASA leo jijini Dar es salaam.



No comments:

Post a Comment