Wednesday, December 16, 2015

MWILI DOTTO WA JAMII FORUMS WASAFIRISHWA KWENDA SAME


Jeneza lenye Mwili wa Marehemu Dotto Mzava likishushwa Kwenye gari maalum mara baada ya kuwasili katika kanisa la Wasabato Manzese uzuri kwaajili ya sala ya kuombea kabla ya Mwili kusafirishwa kuelekea Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro.



Mchungaji wa kanisa la Adventist wasabato akiendelea na ibada wakati wa ibada ya kumuombea marehemu kabla ya kusafirishwa kuelekea Same Kilimanjaro


Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Jamii Media Maxence Mello akitoa historia fupi ya Marehemu Dotto Mzava ambae pia alikua mmoja wa watumishi katika kampuni hiyo.


Baba Mkubwa wa marehemu Dotto Mzava akitoa maneno ya shukrani katika kanisa la Kisabato la Manzese Uzuri mara baada ya zoezi la misa kumalizika.




Heshima za Mwisho zikiendelea kutolewa




Majonzi na simanzi kwa ndugu wa marehemu




Mmiliki wa Fullshangwe Blog,John Bukuku akitoa heshima za mwisho




Heshima za mwisho zikiendelea kutolewa kwa mwili wa marehemu Dotto Mzava kabla haujasafirishwa kuelekea Same Kilimanjaro kwaajili ya mazishi




Mbunge wa Jimbo la Kibamba, John Mnyika akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa marehemu Dotto Mzava kabla ya Kusafirishwa kuelekea Same Kilimanjaro kwa mazishi yanayotarjiwa kufanyika kesho




Mkurugenzi mtendaji wa Jamii Media akitoa heshima za mwisho kabla ya mwili wa marehemu kusafirishwa Same Mkoani Kilimanjaro mapema leo




Ibada ikiendelea








Jeneza lenye mwili wa marehemu Dotto Mzava likipandishwa ndani ya gari tayari kwa safari ya kuelekea Same Mkoa wa Kilimanjaro leo kwaajili ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho




Ndugu, jamaa na marafiki wakiwa kanisani




Kwaya ya Angaza ikitoa huduma wakati wa ibada ya kumuombea marehemu Dotto Mzava




Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Dotto Mzava wakiwa kanisani kwenye ibada ya kumuombea marehemu iliyofanyika katika kanisa la Wasabato la Manzese Uzuri kabla ya Mwili kusafirishwa kwaajili ya kwenda kupumzishwa katika nyumba yake ya milele huko Kwao Same Mkoa wa Kilimanjaro.Picha na Pamoja Blog

No comments:

Post a Comment